Availability: In Stock

KURUNZI YA KISWAHILI GREDI YA 2

SKU: 9789966573728

Kshs 597.00

Kurunzi ya Kiswahili Kitabu cha Mwanafunzi Gredi yo Pili kimeandaliwa kwa ustadi ili kumwezesha. mwanafunzi kumudu mtaala mpya 2017 unaolenga umilisi kwa njia sahili, yenye mvuto na ya kumjumuisha moja kwa moja kwenye shughuli za ufunzaji.

Sifa za kitabu hiki:

  • Kimeshughulikia mada kwa namna ambayo inamwezesha mwanafunzi kushiriki kikamilifu katika ujifunzaji.
  • Mada na shughuli za darasani zimeteuliwa kwa uangalifu kumjengea mwanafunzi umilisi wa aina mbalimbali.
  • Kuna mazoezi na mijarabu anuwai (mazoezi, shughuli kwa mwanafunzi, miradi, mijarabu ya mwisho wa mada) kumwezesha mwalimu kupima umilisi wa mwanafunzi wa stadi mbalimbali za lugha.
  • Picha halisi na michoro ya kuvutia zinazosaidia katika uelewa wa mada.
  • Kinalenga kumsaidia mwanafunzi kutumia wifaa vya tekrrolojia kama vile video, redio, tabuleti katika kurahisisha ujifunzaji.
  • Mbinu tofauti za ufunzaji zimejumuishwa kama vile miradi shambani, shughuli nje ya darasani katika jamii (shambani, dukani, sokoni, usafi), kumwalika mgeni (wa usalama, usafi, mtaalamu), kutumia nyimbo, mashairi, kumhusisha mzazi au mlezi, uchoraji na ujifunzaji katika vikundi. Mbinu hizi zinasaidia kujenga umilisi wa mwanafunzi.
  • Masuala mtambuko na kuhusisha maadili kujenga mada tofauti imeshughulikiwa.
  • Kitabu cha mwalimu kipo ili kumpa mapendekezo katika ufunzaji.